Kwa vijana
För tonåringar – swahili
Kwa vijana, miaka 13 hadi 18.
Haki zako kama mtoto nchini Uswidi
Nchini Uswidi unachukuliwa kuwa mtoto hadi ufike umri wa miaka 18. Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Mtoto, unaoitwa Mkataba wa Watoto, ni sheria nchini Uswidi. Mkataba wa Haki za Mtoto unasema haki ambazo watoto wote wanazo. Pia kuna sheria nyingine nchini Uswidi zinazolinda watoto. Hapa unaweza kusoma kuhusu baadhi ya haki na sheria maalum zilizopo ili kuwalinda watoto.
Watoto wote wana haki ya kuwa huru kutokana na dhuluma. Hakuna mtu mzima anayeweza kukupiga, kukupiga teke, kukusukuma, kuvuta nywele zako au kukutishia.
Wasiliana na polisi kwenye simu 114 14 ikiwa unadhulumiwa.
Ukiwa hatarini, piga simu 112.
Tembelea tovuti ya kutahadharisha ya SOS sosalarm.se External link.
Ndoa za utotoni ni marufuku
Katika nchi mbalimbali kuna vikomo tofauti vya umri unapozingatiwa kuwa mtu mzima na unapozingatiwa kuwa mtoto. Sheria za kuolewa hutofautiana kati ya nchi mbalimbali.
Nchini Uswidi wewe ni mtoto hadi siku unapofikisha umri wa miaka 18, na kabla ya hapo huwezi kuolewa.
Hii ni kwa sababu inaaminika kwamba mtoto hapaswi kubeba jukumu linaloambatana na kuishi katika ndoa. Ndoa za utotoni zinaweza kusababisha watoto kujihisi vibaya kimwili na kisaikolojia kwa sababu mtoto anaweza kuathiriwa katika ukuaji wake kama mtu binafsi na kuishi maisha anayostahili.
Unapofika umri wa miaka 18, unaweza kuamua iwapo unataka kuolewa na ikiwa ndivyo, na nani. Hakuna mtu anayeweza kumlazimisha au kumdanganya mtu yeyote kwenye ndoa. Ni kinyume cha sheria kujaribu kumlazimisha au kumdanganya mtoto kusafiri kwenda nchi nyingine kuolewa. Pia ni uhalifu unaoweza kusababisha kifungo. Pia ni kinyume cha sheria kumlazimisha mtoto kuishi katika uhusiano unaofanana na ndoa. Wakati mtu mzima anafanya ngono na mtoto aliye chini ya umri wa miaka 15, inazingatiwa kuwa ubakaji.
Ikiwa mtu yuko chini ya umri wa miaka 18 na ameolewa
Ikiwa mmoja wa mwanandoa alikuwa chini ya umri wa miaka 18 alipoolewa, ndoa hiyo itabatilishwa nchini Uswidi.
Ikiwa uko chini ya umri wa miaka 18 na unaomba hifadhi pamoja na mtu uliyeolewa naye, badala ya kuwa na wazazi wako, unachukuliwa kuwa mtoto asiyeandamana na mtu mzima. Kisha utapata mlezi ambaye atakusaidia kuwasiliana na mamlaka.
Hapa unaweza kumgeukia
Ikiwa una maswali au unahitaji msaada, unaweza kuzungumza na mwalimu, mshauri au mhudumu. Unaweza pia kutumia Swedish Migration Agency au huduma ya ustawi wa kijamii ya manispaa. Ikiwa una mlezi, unaweza pia kumtegemea.
Iwapo unaogopa kwamba wewe au mtu unayemjua ataolewa, unaweza kupiga simu kwa polisi kwenye nambari 114 14.
Ukeketaji wa wanawake ni marufuku
Ukeketaji wa wanawake au tohara ya wanawake kama wengine wanavyouita, hutokea katika sehemu nyingi ulimwenguni. Ukeketaji wa wanawake ni pale unapokata au kushona sehemu nyeti ya nje ya msichana au kuiharibu kwa njia nyingine. Hakuna mtu anayeruhusiwa kufanya utaratibu kama huo kwa msichana, hata ikiwa imekuwa desturi katika familia.
Ukeketaji wa wanawake ni marufuku kabisa nchini Uswidi na huchukuliwa kuwa uhalifu mkubwa. Mtu yeyote ambaye amekeketwa hataadhibiwa.
Wasiliana na polisi kwa simu 114 14 ikiwa unaogopa kwamba wewe au mtu unayemjua atakeketwa. Unaweza pia kupiga simu kwa nambari ya usaidizi wa kitaifa wa wanawake wa Uswidi (Kvinnofridslinjen) kwenye 020-50 50 50 ili upate ushauri na usaidizi. Kvinnofridslinjen nambari ya usaidizi wa kitaifa wa wanawake ambao wamekabiliwa na vitisho au dhuluma.
Ukeketaji wa wanawake – tohara ya sehemu nyeti za wasichana - 1177 (kwa Kiswidi) External link.
Youmo – Nimechanganywa kiasili, ninawezaje kupata msaada? (kwa Kiswidi) External link.
Una haki ya kuepuka dhuluma na ukandamizaji unaohusiana na heshima
Katika baadhi ya familia na koo, ni muhimu kwamba hakuna sifa mbaya kuhusu familia. Kunaweza kuwa na sheria kuhusu nguo ambazo mtu anaweza kuvaa, ni nani unayeweza kuchangamana naye, kwamba huwezi kuwa pamoja na kuoa mtu unayetaka au kusoma na kufanya kazi na kile unachotaka.
Sheria hizi huwa kali zaidi kwa wasichana, lakini pia kuna sheria zinazotumika kwa wavulana. Ikiwa sheria zinakufanya utendewe vibaya au kuadhibiwa, inaitwa unyanyasaji au ukandamizaji unaohusiana na heshima. Baadhi yao wanaweza kuchapwa, kutishiwa au kuitwa majina mabaya. Kumpitisha mtu kwa hii kunakiuka Mkataba wa Haki za Mtoto na sheria ya Uswidi.
Wakati fulani watoto hulazimika kuwaangalia ndugu zao kwa sababu familia ina wasiwasi kwamba uvumi utaenezwa kuwahusu. Lakini watu wote wana haki ya kuishi maisha yao jinsi wanavyopenda. Hii inatumika bila kujali dini au utamaduni wa mtu na nchi au familia yake. Watoto wote wana haki ya kuishi maisha yao na hawapaswi kumdhibiti mtu mwingine.
Hapa unaweza kumgeukia
Ikiwa wewe au mtu unayemjua yuko katika mazingira magumu, unaweza kumwendea mwalimu wa shule yako, huduma ya ustawi wa kijamii katika manispaa yako au Swedish Migration Agency ili upate msaada. Pia kuna mashirika mbalimbali yanayotoa usaidizi na taarifa kuhusu dhuluma na ukandamizaji unaohusiana na heshima.
GAPF – Riksorganisation mot hedersvåld (kwa Kiswidi) External link.: Hapa unaweza kupata usaidizi ikiwa wewe mwenyewe au mtu mwingine anafanyiwa dhuluma au ukandamizaji unaohusiana na heshima. Unaweza kupiga simu 08-711 60 32, barua pepe au gumzo.
Kärleken är fri (kwa Kiswidi) External link.: Hapa unaweza kupata usaidizi kupitia gumzo na barua pepe ikiwa una maswali kuhusu dhuluma au ukandamizaji unaohusiana na heshima, haki, mapenzi, ndoa ya kulazimishwa au ukeketaji.
Tris – Tjejers rätt i samhället (kwa Kiswidi) External link.: Hapa unaweza kupata usaidizi ikiwa unahisi kuwekewa vikwazo na familia au jamaa zako, au unatishiwa au kudhulumiwa unapojaribu kufanya maamuzi yako mwenyewe. Piga simu 010-255 91 91.
Usawa wa watu wote
Nchini Uswidi, kuna sheria kadhaa zinazohusika na ukweli kwamba watu wote wana thamani sawa na haki sawa. Tunapaswa kuwa na haki na fursa sawa bila kujali sisi ni nani, jinsi tulivyo, tunakotoka, tunachoamini, tunayempenda au jinsi tunavyofanya kazi.
Kuna sheria za kumzuia mtu kubaguliwa au haki zake kukiukwa. Kama binadamu, tunaruhusiwa kuhisi, kufikiri na kuamini tunavyotaka lakini haturuhusiwi kufanya chochote. Imeelezwa katika katiba kwamba watu wote wana haki ya kueleza mawazo yao, maoni na hisia mradi tu hawamuudhi mtu mwingine yeyote. Ni lazima sote tuheshimu haki ya binadamu wenzetu ya utambulisho wao na machaguo ya maisha.
Usawa wa kijinsia
Usawa unamaanisha kwamba wavulana na wasichana wanapaswa kuthaminiwa kwa usawa na kuwa na fursa sawa maishani. Pia inamaanisha kwamba wanaume na wanawake watu wazima lazima wawe na haki na wajibu sawa. Lazima wawe na uwezo sawa wa kuathiri jamii na maisha yao wenyewe.
Miaka 100 iliyopita haikuwa hivyo nchini Uswidi. Wakati huo, wanawake hawakuwa na ushawishi mkubwa wa kujieleza katika maisha yao. Wengi wa waliosoma na kufanya kazi walikuwa wanaume, huku wanawake wakikaa nyumbani na kuwalea watoto, kufanya usafi na kufua nguo. Tangu wakati huo, mengi yamebadilika.
Katika familia nyingi nchini Uswidi leo, wazazi wote wawili hufanya kazi na kusoma na watoto wako katika shule ya chekechea, shule na kituo cha baada ya shule wakati wa mchana. Nyumbani, wazazi wote wawili mara nyingi husaidiana kufanya usafi, kuosha, kufanya ununuzi na kupika, na kuwalea watoto pamoja,
Ili jamii iwe na haki kadiri iwezekanavyo na kuwapa wanawake na wanaume uwezo sawa wa kuathiri jamii na maisha yao wenyewe Riksdag ya Uswidi imeamua kuhusu malengo mbalimbali ya usawa.
Malengo yanahusu
- wanaume na wanawake lazima wawe na fursa sawa ya kujitegemea kifedha ili kwamba hakuna mtu anayemtegemea mwingine kifedha
- wavulana na wasichana lazima wapate ufikiaji sawa wa elimu na haki ya kuchagua kile wanachotaka kusomea
- wanaume na wanawake lazima wawe na fursa sawa ya kuamua kuhusu miili yao wenyewe na unyanyasaji wa wanaume dhidi ya wanawake unapaswa kukoma
- kazi inayofanyika nyumbani lazima igawanywe kati ya wanaume na wanawake. Inamaanisha kwamba akina dada na kaka katika familia moja wanapaswa kusaidia pia vivyo hivyo katika mambo yanayohitaji kufanywa.
Utambulisho wa kijinsia na mwelekeo wa kingono
Nchini Uswidi, kila mtu ana haki ya utambulisho wake mwenyewe wa kijinsia na mwelekeo wa kingono. Utambulisho wa kijinsia unahusu jinsia unayohisi, bila kujali kile ambacho wengine wanatarajia. Mwelekeo wa kingono unahusu jinsia ambayo mtu anavutiwa na kupenda. Una haki ya kupenda na kuwa na yeyote unayetaka, bila kujali iwapo mtu huyo ni wa jinsia sawa au tofauti na yako.
Ikiwa hutaki, huna wajibu wa kufichua kwa wengine mwelekeo wako wa kingono au utambulisho wako wa kijinsia. Hakuna mwelekeo wa kingono au utambulisho wa kijinsia unaovunja sheria, lakini ni kinyume cha sheria kumtendea mtu kwa njia isiyo ya haki au mbaya zaidi, kwa mfano shuleni au katika shirika, kwa sababu ya mwelekeo wa kingono au utambulisho wa kijinsia wa mtu huyo.
Hapa unaweza kumgeukia
Kuna mashirika kadhaa tofauti na mapokezi ya vijana unayoweza kugeukia ikiwa unataka kupata maelezo zaidi au unahitaji usaidizi.
RFSL (kwa Kiswidi) External link.
Kupitia shirika hili unaweza kuungana na watu wengine wa LGBTQI, kushiriki katika shughuli mbalimbali na kupata usaidizi. Pia wana mtandao wa watu ambao ni wageni nchini Uswidi, RFSL Newcomers (kwa Kingereza) External link..
UMO – kuhusu ngono, afya na mahusiano (kwa Kiswidi) External link.
UMO ni tovuti ya kila mtu mwenye umri wa miaka 13–25 ambapo unaweza kusoma zaidi kuhusu mwelekeo wa kingono na utambulisho wa kijinsia.
Ubaguzi wa rangi
Ubaguzi wa rangi huchukulia kwamba watu wanaweza kugawanywa katika vikundi tofauti na kwamba watu wa vikundi fulani hawana thamani. Inaweza, kwa mfano, kuwa kuhusu kugawanya watu kulingana na rangi ya ngozi, utamaduni au dini.
Nchini Uswidi kuna sheria za kuwalinda watu dhidi ya kuathiriwa na ubaguzi wa rangi. Kwa mfano ni marufuku kumnyima mtu kazi au makazi kwa sababu ya jina au asili ya mtu. Pia ni marufuku kuvaa vito na nguo zilizo na swastika, maandishi au ishara nyingine ambazo ni za ubaguzi wa rangi au za kukera kikundi fulani. Pia hairuhusiwi kueneza taarifa kwamba kikundi au mtu hana thamani kwa sababu ya, kwa mfano, rangi ya ngozi au dini.
Wakati mwingine unapotendewa vibaya, inaweza kuwa ngumu kujua iwapo kile ambacho unapitia ni kinyume cha sheria au la. Zungumza na mtu unayemwamini kuhusu kilichotokea, kama vile mwalimu au mtu mwingine unayemwamini.
Watoto wasio na wazazi/walezi
Taarifa kwa wewe unayesafiri kwenda Uswidi bila wazazi wako
Umepokea makazi ya kudumu nchini Uswidi na hivi karibuni utasafiri kwenda huko. International Organization for Migration (IOM) hukupa taarifa kuhusu unachohitaji kubeba kwenye safari yako ya kwenda Uswidi. Una hati za utambulisho (kwa mfano, pasipoti ya nchi yako ya asili, kitambulisho au cheti cha kuzaliwa) au hati nyingine muhimu (kwa mfano), vyeti vya shule, alama za shule, kadi za afya au vyeti vya vifo vya jamaa), basi lazima ulete hati halisi.
Nini kinatokea siku ya kwanza?
IOM ina jukumu la kukufikisha salama nchini Uswidi. Utasafiri kwa ndege hadi Uswidi, kisha utalazimika kusafiri zaidi kwa ndege, treni au gari ili ufike kwenye nyumba yako mpya. Mtu anayefanya kazi katika manispaa atakutana nawe katika uwanja wa ndege na kuandamana nawe hadi mahali utakapoishi. Mamlaka ya Uswidi italipia safari yako, na gharama wakati wa safari na baada ya kufika nchini Uswidi, kwa mfano usafiri, chakula na makazi.
Nitaishi wapi?
Nchini Uswidi utaishi na familia au katika malazi ya kikundi pamoja na watoto na vijana wengine. Katika malazi ya kikundi kuna watu ambao watawajibika kwako na ambao wanaweza kukusaidia. Ili kila mtu afurahi na kuwa na wakati mzuri, kutakuwa na sheria za kila mtu kufuata. Sheria moja inaweza kwa mfano kuwa kwamba kunapaswa kuwa na kimya wakati fulani jioni au kwamba chakula cha jioni kinaandaliwa wakati mahususi kila siku.
Ukifika nchini Uswidi pamoja na watu wazima ambao si wazazi wako, au ikiwa una jamaa nchini Uswidi ambao unataka kuishi nao, mamlaka zinaweza kuchunguza ikiwa unaweza kuishi nao au karibu nao.
Naweza kupata usaidizi gani?
Mlezi maalum
Ikiwa wazazi wako hawako nchini Uswidi, kutakuwa na mtu maalum atakayehakikisha kwamba unapata huduma na usalama. Mtu huyo anaweza, kwa mfano, kukusaidia unapowasiliana na mamlaka, kushughulikia fedha zako na kuhakikisha kwamba unaenda shuleni. Mtu huyo atamaliza kazi yake utakapofikisha umri wa miaka 18 kama sheria na umekuwa mtu mzima kwa mujibu wa sheria ya Uswidi.
Huduma ya ustawi wa kijamii
Nchini Uswidi kuna manispaa 290 na kila manispaa ni sehemu iliyoainishwa kijiografia ya Uswidi. Kila manispaa ina shirika linaloongoza ndani ya manispaa na linawajibika kwa shule, utunzaji wa wazee na usaidizi kwa familia.
Huduma ya ustawi wa kijamii ni sehemu ya manispaa na ina jukumu la kusaidia kila mtu anayeishi hapo. Huduma ya ustawi wa kijami huteua mtu ambaye, pamoja nawe, mtafanya mpango wa malazi, shule, utunzaji na mambo mengine ambayo ni muhimu ili maisha yako yawe mazuri nchini Uswidi. Mwasiliani wako pia ana jukumu la kuhakikisha kwamba unapata usaidizi unaohitaji kutoka kwa jamii ya Uswidi.
Shule
Nchini Uswidi, watoto wote wana haki ya kupata elimu na ni ya bure. Shule ya msingi ni ya lazima nchini Uswidi. Hii inamaanisha kwamba lazima uende shule na kuhudhuria madarasa siku tano kwa wiki, Unahitaji kujifunza Kiswidi ili uweze kushiriki kikamilifu katika jamii na baadaye kuweza kupata kazi. Wakati wa saa za shule, unaweza kuzungumza na mwalimu au mshauri wako ikiwa unahitaji msaada au ikiwa huna uhakika kuhusu jambo lolote. Baada ya shule kutakuwa na wakati wa kufanya kazi yako ya nyumbani au kufuatilia kipendwa. Nchini Uswidi, unaweza pia kufanya kazi baada ya saa za shule na wakati wa likizo, kuanzia umri wa miaka 16.
Huduma ya afya
Huduma ya afya ni ya bure kwa watoto nchini Uswidi. Ukiwa mgonjwa, unaweza kuzungumza na daktari au mtaalamu mwingine wa huduma ya afya kuhusu matatizo yako. Wana jukumu la usiri na kwa hivyo hawaruhusiwi kumwambia yeyote kuhusu kilichotokea kati yenu. Wasiliana na muuguzi wa shule yako au kituo cha afya ikiwa unataka kuweka miadi na daktari.
Hapa unaweza kupata mtoa huduma wa afya aliye karibu nawe: www.1177.se/hitta-vard/ (kwa Kiswidi) External link.
Ninaweza kuungana tena na familia yangu?
Ikiwa umetenganishwa na familia yako na unahitaji msaada wa kuwapata, unaweza kuwasiliana na Swedish Red Cross. Wanaweza kukusaidia kutafuta jamaa.
Tovuti yao ni: www.rodakorset.se (kwa Kiswidi) External link.
Ushauri wa simu: 020-415 000
Ukipenda, wazazi na ndugu zako wanaweza kutuma ombi la kukutana tena nawe nchini Uswidi. Kwa kawaida huchukua muda mrefu kuanzia kuwasilishwa kwa ombi hadi upokee jibu, na kuna sheria nyingi tofauti za kuungana na familia.
Soma zaidi kuhusu kuunganishwa tena na familia na jinsi ya kutuma ombi (kwa Kingereza)
Elimu
Nchini Uswidi, ni lazima kwenda shule kutoka shule ya awali hadi sekondari ya juu. Shule ya Uswidi ni bure na chakula cha mchana kinajumuishwa kila siku. Huenda ukahitaji kuhudhuria kinachojulikana kama darasa la maandalizi kabla ya kuanza shule na wanafunzi wa Uswidi. Walimu wako na wafanyikazi wa shule watakuwepo kukuongoza na kukusaidia.
Elimu nchini Uswidi
Kwenda shule ni sehemu muhimu ya kukua nchini Uswidi. Pia utaanza shule baada ya kuhamia nchini Uswidi.
Shule ya Uswidi ina viwango tofauti: darasa la chekechea, shule ya msingi na shule ya sekondari ya juu. Ukiwa na umri wa miaka sita, unaanza shule ya chekechea na mwaka unaofika umri wa miaka kumi na sita, unamaliza darasa la tisa. Kisha shule ya msingi inafika mwisho. Kisha unaweza kuanza shule ya sekondari ya juu, ambapo unaweza kusoma kwa miaka mitatu.
Shule ya upili si ya lazima, lakini ni muhimu kwako kwenda shule ya upili kwa sababu inafanya iwe rahisi kwako kupata kazi. Ili kusoma katika chuo au chuo kikuu, itabiti uende shule ya sekondari ya juu.
Nchini Uswidi, elimu ni ya bure kwa kila mtu. Wavulana na wasichana huenda shuleni pamoja. Mlo wa bila malipo hujumuishwa wakati wa mapumziko ya chakula cha mchana shuleni kila siku. Nchini Uswidi, sare za shule hazivaliwi. Unaamua mwenyewe kile unachotaka kuvaa shuleni.
Kwenda shuleni nchini Uswidi
Unapokuja nchini Uswidi, unawekwa shuleni. Huko, walimu watakisia kwanza maarifa uliyonayo tayari, ili uwekwe kwenye darasa sahihi. Kisha wanapanga kile ambacho utajifunza. Ni kawaida kwa watoto ambao ni wapya nchini Uswidi kuhudhuria darasa la maandalizi kwanza. Katika darasa la maandalizi utajifunza lugha ya Kiswidi na kuhusu utamaduni wa Uswidi.
Kwenda shule ni muhimu kwa watoto na vijana nchini Uswidi. Shuleni utajifunza hisabati, sayansi, masomo ya kijamii, jiografia, michezo na muziki. Wanafunzi wote husoma Kiswidi na Kiingereza.
Una siku za shule kwa wiki na kwa kawaida una kazi ya nyumbani ya kufanya baada ya shule. Siku ya kawaida shuleni huanza karibu saa mbili asubuhi na huisha alasiri. Mbali na kuwa darasani na kujifunza masomo tofauti, utakuwa na mapumziko ya chakula cha mchana na kati ya masomo ambapo unapata kuwajua wanafunzi wenzako.
Shuleni, ni muhimu kwa wanafunzi kuonyesha heshima kwa walimu na pia kwamba walimu waonyeshe heshima kwa wanafunzi. Unaweza kutumia majina ya kwanza ya walimu wako unapozungumza nao. Ni jambo la kawaida kwa wanafunzi kuzungumzia mada tofauti kwa uwazi na walimu.
Nchini Uswidi, elimu ya watoto si jukumu la shule pekee. Wazazi walezi pia wana jukumu muhimu. Walimu huwa na mikutano ya mara kwa mara na wanafunzi na wazazi/walezi kuzungumza kuhusu jinsi kazi yao ya shule inavyoendelea na jinsi mwanafunzi anavyoweza kupata msaada anaohitaji.
Walimu wanaweza pia kuzungumza na mwalimu na wazazi wake ikiwa mwanafunzi huyo hafuati sheria shuleni. Hakuna mwalimu shuleni anayeweza kutumia dhuluma dhidi ya mwanafunzi. Wakati mwanafunzi hafuati sheria za shule, kuna njia nyingine za kutatua.
Unaweza kupokea usaidizi wakati wa masomo yako
Ni muhimu kwamba vijana wajisikie vizuri. Ndiyo maana shule za Uswidi zina wafanyakazi maalum wanaoweza kukuongoza na kukusaidia wakati wa masomo yako. Kwa mfano, kuna washauri na wauguzi wa shule wa kuzungumza nao ikiwa una matatizo au maswali kuhusu masomo yako, marafiki au familia. Wana wajibu wa usiri kuhusu kile ulichowaambia. Hii inamaanisha kwamba unaweza kuzungumza na mshauri au muuguzi wa shule kuhusu mambo ambayo huwezi kuthubutu au hutaki kuzungumza na familia au marafiki zako.
Mbali na kukusaidia na hali yako ya kiakili na kimwili, shule pia zina mshauri wa masomo. Mshauri wa masomo anaweza kukusaidia kujua unachotaka kufanya baada ya kumaliza shule. Wanaweza pia kukusaidia kutuma maombi ya elimu ya juu na kukuambia kuhusu kazi tofauti na machaguo ya taaluma.
Elimu ya juu
Unapomaliza shule ya msingi, unapendekezwa kuendelea kusoma katika shule ya sekondari. Kuna mipango mingi tofauti ya shule ya sekondari yenye utaalamu tofauti wa masomo. Inakupa fursa ya kujifunza kitu ambacho unapendelea sana.
Maswali ya kufikiria na kuzungumzia:
- Shule hufanya kazi vipi katika nchi yako ya asili? Je, kuna tofauti au mifanano gani hapo ikilinganishwa na Uswidi?
- Je, una mpango wa kile unachotaka kusomea au kufanya kazi katika siku zijazo?
Marafiki na mahusiano
Kukutana na marafiki wapya ni njia rahisi kwako kuingia katika jamii ya Uswidi. Inafurahisha kuchangamana na marafiki na wanaweza pia kuwa wa usaidizi mzuri kwako unapokuwa mgeni nchini Uswidi. Kupitia marafiki utapata jumuiya katika nchi yako mpya na unapoishi. Pia ni njia nzuri ya kufanya mazoezi ya lugha ya Kiswidi.
Jinsi unavyoweza kukutana na marafiki wapya
Kukutana na marafiki wapya katika nchi mpya kunaweza kuonekana kuwa ngumu mwanzoni. Eneo moja unapoweza kukutana na marafiki wapya ni shuleni, ambapo unaweza kutangamana na wanafunzi wenzako wapya na wanafunzi wengine kila siku. Nchini Uswidi, ni jambo la kawaida kwa watu kuendelea kuchangamana hata baada ya mwisho wa siku ya shule katika nyumba ya kila mmoja, katika kituo cha burudani au kupitia shughuli mbalimbali. Nchini Uswidi, watoto na vijana huchangamana bila kujali jinsia, dini au nchi ya asili.
Wengi watakutana na marafiki kupitia vipendwa vya kawaida. Mifano ya vipendwa hivyo inaweza kuwa michezo, muziki, filamu na kusoma. Kuna vyama vya michezo unavyoweza kujiunga navyo na maeneo mengine ya kukutana kwa ajili ya vipendwa tofauti.
Marafiki mtandaoni
Watu nchini Uswidi wamezoea kutumia teknolojia na intaneti katika maisha yao ya kilas siku. Marafiki wanaokutana kwa kawaida huwasiliana kwa kupiga simu, kutuma ujumbe wa maandishi na kukutana katika majukwaa mengine ya kawaida mtandaoni. Baadhi yao hujumuika katika maisha halisi na mtanaoni na wengine huchangamana mtandaoni pekee. Kucheza michezo mtandaoni ni njia ya kawaida ya kukutana na marafiki.
Fikiria kuhusu hii
Ingawa inafurahisha kupata marafiki wapya na kuzungumza na watu mtandaoni, kuna baadhi ya sheria rahisi ambazo kila mtu anapaswa kufuata.
- Picha na ujumbe: Si kila mtu ndiye alivyojitambulisha mtandaoni. Kwa hivyo ni muhimu kufikiria kabla ya kutuma Picha na ujumbe wa maandishi mtandaoni. Kwa mfano, ikiwa umetuma picha, huwezi kuathiri jinsi inavyotumiwa na wengine.
- Nenosiri: Kamwe usifichue manenosiri yako. Ikiwa nenosiri lako limeshirikiwa na mtu mwingine, unapaswa kubadilisha nenosiri lako.
- Kuwa mwangalifu ikiwa utakutana na mtu ambaye hujawahi kutana naye hapo awali. Kamwe huwezi kuwa na uhakika kwamba mtu huyo ndiye aliyejitambulisha mtandaoni.
- Kuwa mwangalifu jinsi unavyojieleza katika ujumbe wa maandishi, au kile unachoandika kuhusu wengine. Ujumbe wa maandishi unaweza kufasiriwa kwa njia tofauti na watu tofauti na kwa hivyo unaweza kuumiza, hata ikiwa haikuwa nia yako.
Marafiki na mahusiano nchini Uswidi
Watu wa jinsia na asili tofauti mara nyingi huchangamana nchini Uswidi. Urafiki unaweza kuonekana kuwa tofauti. Jambo la kawaida kwa wote ni kwamba unaonyesha fadhili na kupendezwa na kila mmoja.
Kuwa mwenye fadhili na kupendezwa kunaweza katika visa fulani kumaanisha kwamba kunaweza kuwa na uhusiano wa kimapenzi lakini pia kunaweza kuwa ishara ya urafiki. Ikiwa huna uhakika kuhusu uhusiano ulionao, ni muhimu kwamba uzungumze na mhusika.
Ridhaa ni muhimu
Ikiwa unaanza uhusiano wa kimapenzi na mtu mwingine, ni muhimu kuheshimu mapenzi ya mtu huyo, pamoja na yako pia. Ridhaa inamaanisha kwamba watu wote wawili katika uhusiano lazima watake kushiriki, kwa mfano, katika tendo la ngono. Ikiwa mtu mmoja hataki, hiyo inamaanisha kwamba yule mwingine lazima akubali.
Soma zaidi kuhusu ridhaa (kwa Kiswidi) External link.
Soma zaidi kuhusu ngono, mwili na afya (kwa Kingereza) External link.
Uonevu
Uonevu unaweza kuwa wa kimwili na wa kisaikolojia na unaweza kupatikana shuleni, wakati wa burudani na mtandaoni. Uonevu unamaanisha mtu kumpiga au kumuumiza mtu mwingine, kusema mambo ya kudhalilisha na kueneza uvumi. Inaweza pia kumaanisha kumfanya mtu mwingine ahisi kutengwa au kutokubalika.
Ikiwa wewe au mtu mwingine anaonewa, unaweza kuzungumza na mwalimu, mshauri wa shule au mtu mzima mwingine unayemwamini na kumwambia kilichotokea.
Maswali ya kufikiria na kuzungumzia:
- Una vipendwa vyovyote? Je, unawezaje kupata watu wenye nia moja kushiriki kipendwa chako?
- Je, kuna tofauti zozote kati ya jinsi mahusiano yanavyofanya kazi nchini Uswidi, ikilinganishwa na kile ulichozoea?
Kiswidi | Kiingereza | Kiswidi |
|---|---|---|
Karibu | Welcome | Välkommen |
Hujambo | Hello | Hej |
Habari zako? | How are you? | Hur mår du? |
Nzuri | I am fine | Jag mår bra |
Asante | Thank you | Tack |
Karibu | You are welcome | Varsågod |
Tafadhali | Please | Snälla |
Samahani | Sorry | Förlåt |
Unaitwaje? | What is your name? | Vad heter du? |
Jina langu ni … | My name is ... | Jag heter ... |
Sielewi | I do not understand | Jag förstår inte |
Sizungumzi Kiswidi | I do not speak Swedish | Jag pratar inte svenska |
Kwaheri | Goodbye | Hej då |